19 November 2010
Dk Slaa na kura zake
Aliyekuwa mgombea urais wa chadema, Dk Wilbroad Slaa akipiga kura--- Je na kura yake hii ilichakachukuliwa Karatu.
vijana wa CCM hawataki viongozi wa ccm wilaya arusha
pichani ni baadhi ya vijana wa CCM wilaya ya arusha wakiandamana kutowataka viongozi wa CCM wilaya ya Arusha kwa tuhuma za kumuhujumu aliyekuwa mgombea ubunge wa CCM jimbo la Arusha Dk Batilda Burian ambaye alishindwa na mgombea wa chadema Godbless Lema.
mfanyabiashara wa ndizi mto wa mbu
Bibi huyu ni mfanyabiashara wa ndizi katika mji wa mto wa mbu wilayani Monduli- jimbo la aliyekuwa waziri mkuu Edward Lowassa
siasa za karatu ndio hizi
JK alipofika karatu kwenye kampeni, alipokelewa na mamia ya vijana wakiwa wamevaa fulana za CCM, wengi hawakuelewa na kuna magazeti yaliandika JK avunja ngome ya chadema karatu, ila hapa ni vijana wale wale wakiwa katika maandamano ya kumpongeza mbunge mteule wa chadema karatu, mchungaji Israel Yohana Natse.
Subscribe to:
Posts (Atom)