17 December 2010
05 December 2010
VITA dhidi ya UKIMWI na wanahabari
pichani ni waliokaa kwenye viti ni mbunge jimbo la Arusha,chadema Godbless Lema akiwa na mbunge chadema viti maalum mkoa Arusha ,Joyce Mukya, meneja wa PSI mkoa wa Arusha na Manyara, Chris Mbajo, mratibu wa TACAIDS mkoa wa Arusha na Mkurugenzi wa kampuni ya Ms Unique Mussa juma na mratibu wa semina Upendo Simwita ,picha hii ilipigwa mara baada ya kufunguliwa na Lema semina ya waandishi wa habari mkoa wa Arusha kuhusiana na ugonjwa wa UKIMWI semina hiyo iliandaliwa na kampuni ya ms unique promotion ya Arusha
03 December 2010
Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania, Dietlof Mare akimshukuru na kumpongeza Elifuraha Paul Mtowe mfanyakazi mwanzilishi wa Vodacom katika Kanda ya Kaskazini ya Tanzania ambaye amehusika kwa kiasi kikubwa kufundisha huduma za kampuni hiyo kwa umma, kukuza biashara, kupanua mawasiliano na kuwajengea wakazi wa Kanda ya Kaskazini Imani kwa Vodacom, Kuipenda, Kuiheshimu na Kuitumia kampuni hiyo katika huduma za mawasiliano hali inayoifanya Vodacom kubakia mtandao mkubwa na unaoheshimika kwa Kanda hiyo na Tanzania kwa ujumla.
wabunge wa chadema na wanahabari mara baada ya semina ya HIV
mbunge wa jimbo la Arusha, Godbless Lema akiwa na mbunge wa viti maalum mkoa wa Arusha, chadema JoyceMukya wakizungumza na baadhi ya waandishi wa habari mkoani Arusha mara baada ya kufungua semina ya masuala ya UKIMWI kwa wanahabari ambayo iliandaliwa na kampuni ya MS unique kwa kushirikiana na TASWA Arusha .
Wanahabari na vita dhidi ya UKIMWI.
WAANDISHI wa habari nchini, wameombwa kujiepusha na vitendo hatarishi ambavyo vinachangia maambukizi dhidi ya ugonjwa wa Ukimwi.
Mbunge wa Jimbo la Arusha,Godbless Lema, alitoa wito juzi wakati akifungua semina ya siku moja ya waandishi wa habari mkoani Arusha juu ya masuala ya UKIMWI ambayo ilifanyika Ricks Morden klabu .
Lema alisema waandishi wa habari kama wanajamii wengine, wanakabiliwa na tishio kubwa la maambukizi ya UKIMWI kutokana na mazingira ya kazi zao.
“nawapongeza waratibu wa semina hii na mimi kama mbunge nawahakikishia tutaendelea kushirikiana wakati wote kama masuala haya ya kijamii”alisema Lema.
Akitoa mada katika semina hiyo,Dk Saimon Megiroo toka hospitali ya Selian mkoani hapa, alisema wanahabari ni wadau muhimu sana katika vita dhidi ya Ukimwi kama wakitumia kalamu zao kuelimisha vyema jamii.
“Selian tuna kitengo cha masuala ya Ukimwi na moja ya wadau wetu katika masuala ya uelimishaji ni wanahabari”alisema Dk Migiroo.
Naye Meneja mahusiano ya shirika la mtandao wa wafugaji PINGOS Forum Stivin Shikuku akitoa mada katika semina hiyo, alisema jamii za wafugaji bado zinaathirika sana na ukimwi kutokana na kutokuwa na elimu ya kutosha.
Akitoa mada juu ya tafiti za vita dhidi ya UKIMWI katika jamii hizo, alisema bado huduma muhimu za afya kama upimaji na upatikanaji wa dawa za kurufusha maisha katika jamii hizo hazipatikani.
Awali Meneja wa shirika la PSI mkoa wa Arusha na Manyara, Chris Mbajo akitoa mada yake juu ya kujikinga na maambukizi mapya ya UKIMWI aliwataka wanahabari kuhakikisha wanajiepusha na vitendo vitakavyo wafanya wapate maambukizi.
Semina hiyo ya wanahabari iliyodhaminiwa na mamlaka ya hifadhi Ngorongoro, shirika la wafugaji la Pingos Forum, iliandaliwa na chama cha waandishi wa michezo mkoa Arusha(TASWA) kwa ushirikiano na kampuni ya Ms Unique na chama cha wanaoishi na virusi cha Tumaini Positive(TUPO).
MWISHO.
baraza la mawaziri la maridhiano ndani ya CCM lina jipya
Tutegemee nini Baraza la mawaziri la maridhiano ndani ya CCM.
Mussa Juma.
MAWAZIRI 50 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , wameapishwa ,huku kukiwa na sura mpya 24 na sura zilizozoeleka ndani ya baraza hilo 26.
Uteuzi huu ambao umefanywa na Rais Jakaya Kiwete, umepokelewa kwa hisia tofauti na wadau mbali mbali wa masuala ya siasa, wapo walipongeza, wapo walioomba mawaziri kupewa muda na wapo ambao wanaamini baraza hili ni vigumu kutekeleza Ilani ya uchaguzi wa CCM.
Wanaotilia shaka baraza hili, wanahoja mbali mbali kwanza wanaona bado ni kubwa,pili sura nyingi ni zile zile na pia ahadi za CCM zilikuwa nyingi sana katika uchaguzi uliopita hivyo kutekeleza zote ni ndoto ya mchana.
Lakini kikubwa zaidi katika baraza hili ni kuonekana ni baraza la maridhiano ndani ya CCM kutokana na mawaziri wengi ambao hawakuwa wanamtando kupewa nafasi katika wizara zenye majukumu makubwa.
Uteuzi wa baadhi ya mawaziri na kupewa wizara kubwa nje ya mtandao pia umepokelewa kwa hisia tofauti na wadau wa masuala ya siasa.
Wapo wadau ambao sasa wanaamini Rais Kikwete kaamua kuweka kanda wapiganaji makubwa wa mtandao uliosaidia ushindi wake mwaka 2005 na wapo wanaoamini sasa ameamua kuzima manunguniko ya baadhi ya wanasiasa wakongwe na Wananchi kuhusu uteuzi ambao amekuwa akiufanya.
Baadhi ya Mawaziri ambao wanaaminika hawakuwa katika mtandao na sasa wapo katika wizara nyeti ni kama John Magufuli,ambaye ni Waziri wa Ujenzi, George Mkuchika waziri wa TAMISEMI,Dk Harryson Mwakyembe Naibu Waziri ujenzi,Shamsi Vuai Nahodha waziri mambo ya ndani,Lazaro Nyarandu Naibu waziri wa Viwanda na biashara na wengine kadhaa.
Ingawa kuna mawaziri wengine hawakuwa katika mtandao hata katika baraza lililopita na sasa wamerejeshwa katika uwaziri na kupewa wizara kubwa, kama Profesa Mark Mwandosya, Waziri wa Maji, kuteuliwa kwao kuna ishara kubwa ya muafaka ndani ya CCM.
Ni kweli usiofichika kuwa kuna baadhi ya mawaziri katika baraza lililopita waliokuwa wanamtandao na wengine hawakuwa wanamtandao, walionekana kupwaya sana katika nafasi zao na hata kufikia hatua ya kukosa mvuto katika jamii.
Lakini sasa baraza hili, kuna mawaziri na manaibu wao kadhaa ambazo hawakuathiriwa sana na mtandao na siasa za makundi ndani ya CCM na hivyo kutoa tumaini jipya la kuona baraza la mawaziri linafanyakazi kwa pamoja na kwa ufanisi mkubwa.
Ninanavyo mimi baraza hili la maridhiano ndani ya CCM, linaweza kuwa na mafanikio makubwa kama wote walioteuliwa wakiamua kufanya kazi kwa maslahi ya Umma na kujitenga na siasa za makundi ya awali.
Na pia baraza hili, linaweza kumsononesha Rais Kikwete kama aliyowateua wakiendeleza makundi yao na hivyo kuhujumiana wao kwa wao.
Makundi ndani ya CCM yamekipa chama hicho, msukosuko mkubwa kuanzia ndani ya chama hadi katika bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na hata kusababisha bunge la tisa chini ya aliyekuwa Spika, Samweli Sitta kufikia maamuzi mazito ya kihistoria.
Kwa upande mmoja migongano wa wakubwa hawa ndani ya CCM imekuwa na manufaa kwa wananchi na upande mwingine pia umekuwa na athari kwa wananchi hasa pale miradi muhimu ya kijamii inapotelekezwa kwa kuzingatia tu aliyeasisi hayupo katika kundi Fulani.
Katika mazingira ya sasa kwa baraza hili, wengi hawatarajii tena kuibuliwa mambo mazito ambayo yanaweza kuitikisa serikali ya Rais Kikwete, hii inatokana na muundo wa baraza hili.
Baraza hili linaweza kurejesha nguvu ya CCM katika uchaguzi mkuu ujao mwaka 2015 au kukimaliza chama hicho, hasa pale mawaziri hawa na wabunge wote wa CCM watakapoamua kusimama kidete na kutetea maslahi ya chama chao badala ya maslahi ya umma.
Uteuzi huu pia unaweza ukawa mwisho wa umaarufu wa waliokuwa wabunge wapiganaji dhidi ya ufisadi kama, Waziri wa Afrika ya Mashariki, Samweli Sitta na Naibu waziri wa Ujenzi Dk Harryson Mwakyembe. kama watakuwa kimya kuzungumza hata yale mambo waliyoyasimamia na kuyapinga katika bunge lililopita.
Hata hivyo, bado ni imani ya wengi kuwa, mawaziri hawa 50 licha ya kuwa mawaziri watatetea maslahi ya umma kwa nguvu zao zote na kujitenga na kutumia nafasi zao kwa manufaa yao .
Mawaziri hawa, wananafasi kubwa ya kubadilisha historia ya taifa hili, pale watakaporuhusu mijada muhimu bungeni na kutoa majibu yenye tija katika masuala ya msingi yanayolalamikiwa na watanzania.
Miongoni mwa mambo hayo ni kuhakikisha watanzania wananufaika na rasilimali za nchi yao, kuhakikisha Tanzania inakuwa na katiba mpya na pia kuhakikisha vita dhidi ya vitendo vya Rushwa na ufisadi, madawa ya kulevya, matumizi mabaya ya madaraka vinapiganwa kwa dhati na sio kwa maneno matupu.
Lakini kama baraza hili,litarejea kule tulipotoka katika siasa za makundi,siasa za kutetea maslahi binafsi, siasa za kuchafuana ni wazi matarajio ya walio wengi yatakuwa yametoweka na baraza hili halitakuwa tena baraza la maridhiano ndani ya CCM bali litaongeza mpasuko.
mussa juma ni mwandishi wa mwananchi mkoa wa Arusha, anapatikana 0754296503 email mussa_juma@yahoo.com,mussanews.blogspot.com
MWISHO.
25 November 2010
kampeni za udini katika siasa za tz
Tutegemee vyama vya kianglikana na kianswar sunna uchaguzi ujao
Mussa Juma
IMEKUWA ni kawaida kila wakati wa uchaguzi kuibuliwa hisia za kidini miongoni mwa vyama vya siasa na wagombea.
Hisia hizo za kidini, zimekuwa zikitumiwa kama mtaji wa vyama pale ambapo chama kimoja kitakapotuhumiwa ni cha kidini.
Kwa bahati mbaya sana propaganda za siasa za kidini zimekuwa zikitumiwa kudhoofisha vyama vya upinzani hasa pale chama kimoja kinapoonekana kuwa na nguvu.
Dhana ya udini ilianza kupamba moto katika chaguzi za mwaka 2005 pale ilipotumika kukidhoofisha chama cha wananchi CUF baada ya kukituhumu kuwa ni cha kiislam.
Katika uchaguzi wa mwaka huu, tuhuma zile zile zilizopunguza nguvu ya CUF, zimehamia chadema na sasa baadhi ya viongozi wa kisiasa na kidini wamesikika wakikihusisha chama hicho na kikristo.
Bila aibu wala hofu ya kutumia siasa za dini kuwagawa watanzania, baadhi viongozi katika uchaguzi wa mwaka huu, wameweza kutumia dhana hiyo ya udini kwa mafanikio japo si yale yaliyokusudiwa.
Katika siasa hizi za kidini, kwa bahati mbaya zaidi baadhi ya viongozi wa dini wamekuwa wakijikuta wakiingizwa kuzishabikia bila hata wao kufanya tafiti na kujua athari za matamko yao .
Ingawa viongozi hawa wa dini, wanamapenzi na vyama vya siasa lakini baadhi wameshindwa kufisha hisia zao na kuchotwa na wanasiasa na hivyo kutumika kama vipaza sauti vya vyama fulani.
Mara nyingi imetokea baadhi ya viongozi wa dini, kujikuta wakiwa washabiki wa chama tawala na kutoa matamko tata yasiyo ya kidemokrasia na hapo hupongezwa na hakuna ambaye hutamka kuwakosea viongozi hao.
Katika uchaguzi wa mwaka 2005, kuna baadhi ya viongozi wa dini walipaza sauti zao na kutamka kuwa,aliyekuwa mgombea wa CCM wa Urais wa chama tawala ni chaguo la mungu.
Waliopaza sauti hizo walipongezwa kila kona na hakuna ambaye aliwaonya kuwa wanaeneza siasa za kidini.
Wengine walitumia madhabahu yao , kukituhumu chama cha CUF wakati huo ni cha kidini na kuwasihi watanzania kuwa makini na chama hicho.
Hata hivyo, kila baya lina uzuri wake, kuhusisha chama na dini Fulani kumesaidia vyama hivyo kupata wanachama ambao ni watiifu wa dini zinahohusishwa na chama.
Hili lipo wazi tangu ipazwe sauti kuwa CUF ni chama cha waislam kimesaidia maeneo yenye waislam wengi kukiunga mkono chama hicho na hili lipo wazi.
Na katika uchaguzi wa mwaka huu, pale chadema walipohusisha na ni ya kikristo kuna maeneo mengi, kumesaidia wakristo kukipigia kura chama hicho na hata kutwaa majimbo muhimu kama Arusha mjini.
Sidhani kama walivumisha sauti hizi za udini, wamejifunza katika hilo japo kuwa sasa chama cha udini cha mwaka 2005 kimeunda serikali ya umoja wa kitaifa Zanzibar .
Hata hivyo, wakati vyama vya CUF na Chadema vikihusisha na dini chama tawala kimekuwa kisafi hakina dini ni cha kipagani na ni cha wote, lakini je matamko haya yana manufaa.
Kama tukiachia hili tusishangae chaguzi zijazo kuna vyama vitaingizwa katika madhehebu fulani kwani dini mbili tayari zimetumika, sauti zitapazwa chama hiki ni cha Kiangilikana na hiki ni cha Answar Sunna na hapo tutakuwa tumefika pabaya zaidi.
Tukifikishwa katika siasa za madhehebu watatueleza kuwa dhehebu hili linakubali matendo haya na hili ni lazima ufanye matendo haya na hapo tutakuwa tumekwisha watanzania.
Nionavyo mimi kwa ujumla wake kuhusisha chama na dini fulani ni jambo la hatari sana na athari zake ni kubwa kama na vurugu za kidini historia zinaonesha zimekuwa hazidhibitiki tutazame Israel na Palestina na hata tutazame yanayofukuta Sudan na nchi nyingine za Ulaya.
Binafsi sihusishi chama chochote na dini yoyote kwani kihistoria katika mapambano yoyote lazima kupata kwanza wafuasi wa kundi fulani ambao watakuunga mkono zaidi na kuungwa mkono huko hakuna maana ndio msingi wa chama au wapiganaji wote.
Wakati wa kudai uhuru historia inaeleza wazi kuwa Waislam wa jijini Dar es Salaam na Pwani walimuunga sana mkono sana hayati Baba wa Taifa mwalimu Julias Nyerere katika harakati za kudai uhuru .
Baadhi ya Waislam wa Dar es salam walifikia hatua ya kumuingiza msikini hayati Nyerere ,kumchagia sadaka na kufunga kwa ajili yake na hata kumtaka yeye kufunga na hata walimfanyia swala maalum.
Lakini hakuna ambaye alihusisha chama cha TANU kuwa ni chama cha kiislam, japo kuwa wafuasi wake wengi wakati huo hata wale waliokuwa wakimuwezesha Mwalim Nyerere walikuwa waislam.
Hivyo hata sasa binafsi siwezi kusema chama chochote ni cha kidini hivi vyama ni vya watu wenye dini zao, imani tofauti lakini wanamawazo yanayofanana na mitazamo inayofanana katika kufikia malengo ya kushika dola.
Kwa msingi huu hiyo nina matatizo makubwa na baadhi ya viongozi wa kisiasa na kidini ambao katika karne hii ya 21 wanataka kuturejesha katika mawazo na mitizano mgando kwa kuhusisha dini na vyama vya siasa vilivyopo sasa.
Naamini viongozi hawa wanaotulazimisha tuanze kumwamini mtu kwa kupitia dini yake wamefilisika kimawazo na wamekosa jipya la kuwaridhisha watanzania waliowengi ambao maisha yao ni magumu.
Hivyo ushauri wangu ni kwa viongozi wetu wa kisiasa na kidini waache kuzitumia dini kwa maslahi yao , nawasihi sana waache mifumo ya kidemorasia ifanye kazi na hivyo tupate viongozi wiliobora na sio bora viongozi.
Mussa juma ni mwandishi Arusha anapatikana simu 0715 296503, email mussa_juma@yahoo.com,mussanews.blogspoti.com.
mwisho
22 November 2010
NANI KUWA MEYA JIJI LA ARUSHA?
Mussa Juma, Arusha.
MADIWANI watano wa chama cha mapinduzi katika jiji la Arusha, wamejitokeza kuwania nafasi za Meya wa jiji na Unaibu meya wa jiji la Arusha.
Katibu wa CCM wilaya ya Arusha, Salum Mpamba akizungumza na mwananchi jana jioni aliwataja waliochukuwa fomu na kurejesha kwa upande wa Meya ni Paul lota Laizer diwani wa kata ya Baraa, Gaudence Lymo diwani wa Olerien na Paul Mathsen diwani wa kata ya Mushono.
Alisema kwa upande wa Naibu Meya waliochukuwa fomu ni Julias Sekeyani wa kata ya Terati na Alfonce Mawazo wa kata ya Sombetini.
"hadi sasa mwisho wa kuchukuwa fomu ni hao madiwani watano wamejitokeza na tunasubiri vikao vianze kuwajadili na baadaye kupitisha jina moja kwa kila nafasi"alisema Mpamba.
Hata hivyo,.alisema wakati jana ilikuwa mwisho ndani ya CCM kuchukuwa fomu, bado idadi ya viti maalum vya udiwani ambavyo kila chama inapaswa kuvipata haijajulikana.
" ni kweli majina ya viti maalum bado ila majina ya wagombea hawa yanahitajika mapema ili kujadiliwa na vikao"alisema Mpamba.
Wagombea hao, wa CCM wanatarajia kuchuana kwa nafasi ya Umeya, na wagombea wa chadema ambapo tayari jina la Estomii Malla diwani wa kata ya Kimandolu limepitishwa huku nafasi ya unaibu Meya majina matatu yanatajwa ambao ni John Bayo wa kata ya Elerai chadema,diwani wa Michael Kivuyo wa TLP na Charles Mpanda wa cxhadema kata ya kaloleni.
Katika jiji la Arusha CCM ina madiwani 10, chadema 9 pamoja na Mbunge nma Tlp mmoja lakini bado idadi ya viti maalum haijatolewa ambayo inaweza kuongeza idadi ya madiwani wa chadema na hivyo kuongeza halmashauri ya jiji la Arusha
MWISHO
MADIWANI watano wa chama cha mapinduzi katika jiji la Arusha, wamejitokeza kuwania nafasi za Meya wa jiji na Unaibu meya wa jiji la Arusha.
Katibu wa CCM wilaya ya Arusha, Salum Mpamba akizungumza na mwananchi jana jioni aliwataja waliochukuwa fomu na kurejesha kwa upande wa Meya ni Paul lota Laizer diwani wa kata ya Baraa, Gaudence Lymo diwani wa Olerien na Paul Mathsen diwani wa kata ya Mushono.
Alisema kwa upande wa Naibu Meya waliochukuwa fomu ni Julias Sekeyani wa kata ya Terati na Alfonce Mawazo wa kata ya Sombetini.
"hadi sasa mwisho wa kuchukuwa fomu ni hao madiwani watano wamejitokeza na tunasubiri vikao vianze kuwajadili na baadaye kupitisha jina moja kwa kila nafasi"alisema Mpamba.
Hata hivyo,.alisema wakati jana ilikuwa mwisho ndani ya CCM kuchukuwa fomu, bado idadi ya viti maalum vya udiwani ambavyo kila chama inapaswa kuvipata haijajulikana.
" ni kweli majina ya viti maalum bado ila majina ya wagombea hawa yanahitajika mapema ili kujadiliwa na vikao"alisema Mpamba.
Wagombea hao, wa CCM wanatarajia kuchuana kwa nafasi ya Umeya, na wagombea wa chadema ambapo tayari jina la Estomii Malla diwani wa kata ya Kimandolu limepitishwa huku nafasi ya unaibu Meya majina matatu yanatajwa ambao ni John Bayo wa kata ya Elerai chadema,diwani wa Michael Kivuyo wa TLP na Charles Mpanda wa cxhadema kata ya kaloleni.
Katika jiji la Arusha CCM ina madiwani 10, chadema 9 pamoja na Mbunge nma Tlp mmoja lakini bado idadi ya viti maalum haijatolewa ambayo inaweza kuongeza idadi ya madiwani wa chadema na hivyo kuongeza halmashauri ya jiji la Arusha
MWISHO
19 November 2010
Dk Slaa na kura zake
Aliyekuwa mgombea urais wa chadema, Dk Wilbroad Slaa akipiga kura--- Je na kura yake hii ilichakachukuliwa Karatu.
vijana wa CCM hawataki viongozi wa ccm wilaya arusha
pichani ni baadhi ya vijana wa CCM wilaya ya arusha wakiandamana kutowataka viongozi wa CCM wilaya ya Arusha kwa tuhuma za kumuhujumu aliyekuwa mgombea ubunge wa CCM jimbo la Arusha Dk Batilda Burian ambaye alishindwa na mgombea wa chadema Godbless Lema.
mfanyabiashara wa ndizi mto wa mbu
Bibi huyu ni mfanyabiashara wa ndizi katika mji wa mto wa mbu wilayani Monduli- jimbo la aliyekuwa waziri mkuu Edward Lowassa
siasa za karatu ndio hizi
JK alipofika karatu kwenye kampeni, alipokelewa na mamia ya vijana wakiwa wamevaa fulana za CCM, wengi hawakuelewa na kuna magazeti yaliandika JK avunja ngome ya chadema karatu, ila hapa ni vijana wale wale wakiwa katika maandamano ya kumpongeza mbunge mteule wa chadema karatu, mchungaji Israel Yohana Natse.
17 November 2010
breakingnews
Meghji, Nahodha, wateuliwa kuwa wabunge
Shamsi Vuai Nahodha
Zakia Hamdani Meghji
UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
Telephone: 255-22-2114512, 2116539
E-mail: press@ikulu.go.tz
Website: www.mawasilianoikulu.go.tz
Fax: 255-22-2113425
PRESIDENT’S OFFICE,
THE STATE HOUSE,
P.O. BOX 9120,
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais Jakaya Mrisho Kikwete, amefanya uteuzi wa Wabunge watatu (3) kwa mujibu wa Ibara ya 66 (1) (e) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977, kama ilivyorekebishwa na kupewa mamlaka ya kuteua Wabunge 10.
Wabunge walioteuliwa ni Ndugu Shamsi Vuai Nahodha, Prof. Makame Mnyaa Mbarawa na Ndugu Zakia Hamdan Meghji.
Rais atateua wengine waliosalia siku zijazo.
Rais Kikwete ameshawasilisha majina ya wateule hao kwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Anne Semamba Makinda (Mb) kwa ajili ya hatua zipasazo.
MWISHO
Imetolewa na Premi Kibanga,
Mwandishi wa Habari wa Rais Msaidizi,
Ikulu.
Dodoma
17 Novemba
Shamsi Vuai Nahodha
Zakia Hamdani Meghji
UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
Telephone: 255-22-2114512, 2116539
E-mail: press@ikulu.go.tz
Website: www.mawasilianoikulu.go.tz
Fax: 255-22-2113425
PRESIDENT’S OFFICE,
THE STATE HOUSE,
P.O. BOX 9120,
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais Jakaya Mrisho Kikwete, amefanya uteuzi wa Wabunge watatu (3) kwa mujibu wa Ibara ya 66 (1) (e) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977, kama ilivyorekebishwa na kupewa mamlaka ya kuteua Wabunge 10.
Wabunge walioteuliwa ni Ndugu Shamsi Vuai Nahodha, Prof. Makame Mnyaa Mbarawa na Ndugu Zakia Hamdan Meghji.
Rais atateua wengine waliosalia siku zijazo.
Rais Kikwete ameshawasilisha majina ya wateule hao kwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Anne Semamba Makinda (Mb) kwa ajili ya hatua zipasazo.
MWISHO
Imetolewa na Premi Kibanga,
Mwandishi wa Habari wa Rais Msaidizi,
Ikulu.
Dodoma
17 Novemba
15 November 2010
arusha
My Name Mussa Juma(34) Years Old, Journalist Mwananchi news paper Arusha Tanzania .PLZ view news from my blog every day
Subscribe to:
Posts (Atom)